Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bado tunamshikilia Zitto Kabwe - Kamanda Matei

Ijumaa , 23rd Feb , 2018

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe bado anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro toka jana (Alhamisi) kwa tuhuma za kufanya mkusanyiko bila ya kuwa na kibali.

Hayo yameelezwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Ulrich Matei  na kudai wanaendelea na mahojiano nae ili waweze kufahamu alitoa wapi taarifa ya kufanya mkutano ya chama katika maeneo ya nje pamoja na kujua kitu alichokuwa anazungumza na wananchi wa Kata ya Kikeo iliyopo wilayani Mvomero ambapo ndipo alipokamatiwa.

"Ni kweli bado tunamshikilia Zitto Kabwe, tuna muhoji kwa sababu ya kufanya mikutano bila ya kuwa na kibali. Amekwenda kufanya mikutano ya nje maeneo ya hapa Mgeta katika Kata ya Kikeo iliyopo wilayani Mvomero", amesema Kamanda Matei.

Pamoja na hayo, Kamanda Mtei ameendelea kwa kusema "haikuwa inajulikana anazungumzia kitu gani katika mkutano wake, sasa tunajaribu kumhoji ili kuweza kufahamu mazingira yale aliendaje kule na labda alitoa taarifa sehemu gani. Mpaka sasa hivi yupo polisi na suala la dhamana lipo wazi tu anaweza kudhaminiwa muda wowote".

Mbunge Zitto Kabwe pamoja na viongozi wengine wa ACT- Wazalendo tokea  Februari 19 wapo katika ziara ya mikoa nane yenye kata zinazoongozwa na chama hicho kwa malengo ya kushiriki kazi za maendeleo na kuzungumza na kamati za maendeleo za kata hizo.

 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala