Ijumaa , 28th Oct , 2022

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, amesema kuwa serikali imetoa shilingi Bilioni 8 kwaajili ya mafunzo wa ubingwa na ubingwa bobezi kwa watumishi wa umma katika sekta ya afya ili kuondokana na upungufu wa madaktari bingwa ndani ya nchi.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Hayo ameyabainisha hii leo Oktoba 28, 2022, na kusema Tanzania bado inakabiliwa na upungufu wa madaktari bobezi na madaktari bingwa wa magonjwa ya binadamu hali inayosababisha serikali kupeleka baadhi ya wagonjwa nje ya nchi kupatiwa matibabu kwakua hayapatikani katika hospitali za ndani ya nchi.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amesema bado kuna ongezeko la wagonjwa wa afya ya akili na wagonjwa wa mifupa kutokana na ongezeko la ajali za barabarani.