Jumatatu , 3rd Oct , 2022

 Serikali ya Somalia imetangaza kwamba mwanzilishi mwenza na kiongozi mwandamizi wa kundi la kigaidi la  al-Shabab , Abdullahi Nadir, ameuawa jumamosi ya wiki iliyopita huko kaskazini mwa mkoa wa Jubba.

Waziri wa habari  wa Somalia amesema kwamba bwana Nadir alikua ni mkuu wa propaganda za  al Shabab 

 

Taarifa ya waziri huyo imeongeza kwamba al-Shabab ilikua ikimtegemea Nadir kama mrithi wa kiongozi wa sasa wa kundi hilo hatari. aitwae  Ahmed Omar Diriye, maarufu kwa jina la Abu Ubaidah, ambaye taarifa zinasema kwamba ana hali mbaya ya afya. 

Vyombo vya habari vinasema kwamba Nadir alipoteza maisha katika shambulizi la anga. Kwa mujibu wa waziri huyo mashambulizi hayo yalifanywa na vikosi vya usalama nchini Somalia kwa msaada wa majeshi washirika.