
Jafo ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Riziki Shahali Mngwali (CUF) aliyetaka kujua ni kwa nini serikali inaendelea kuwaajiri wakunga wanaume ambao huwazalisha wanawake jambo ambalo ni udhalilishaji kwa wanawake.
Akijibu swali hilo Jafo amesema kwamba serikali itaendelea kuwaajiri wakunga wanaume na wananwake kwa kuwa wote wamefundishwa maadili ya kazi kutoka baraza la wakunga na vilevile hufanya kazi kwa mujibu wa sheria ya ya ukunga ya mwaka 2010.
Aidha Naibu Waziri Jafo amesisitiza kwamba kutafanyika utafiti katika maeneo ambayo mila na desturi zao zinawanyima uhuru kuweza kuhudumiwa na wanaume wakati wa kujifungua ili serikali iweze kuwapanga wanawake wakunga katika maeneo hayo.