Jumanne , 8th Mar , 2022

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema kwamba chini ya uongozi wake kamwe chama chake hakitakuwa ni cha kulipa visasi.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe

Kauli hiyo ameitoa hii leo Machi 8, 2022, mkoani Iringa, wakati akizungumza na Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA), ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

"Nilipopata mwaliko siku ile ile nimetoka gerezani, nikathibitisha nitakwenda, kamwe sikuruhusu uchungu na maumivu binafsi vinipe upofu na kiburi cha kutokuiona heshima niliyopewa na Rais," amesema Mbowe