Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CHADEMA watakiwa kujitokeza kumdhamini Lowassa

Ijumaa , 14th Aug , 2015

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, amewataka wananchi mkoani hapa, kujitokeza kwa wingi jumamosi, kumdhamini Mgombea uras kwa tiketi ya Chama hicho, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Mgombea uras kwa tiketi ya Chama cha Demokrasi na Maendeleo CHADEMA, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Lowassa atawasili mkoani Arusha akitokea uwanja wa Ndege wa kimataifa (KIA), hadi viwanja vya Tindigani Kimandolu atakapokuwa na mkutano wa hadhara.

Aidha mapokezi hayo yatakuwa makubwa na ya historia, yataambatana na ngoma za kila aina ya makabila nchini watakaokuwa wakitumbuiza kuanzia anashuka uwanjani hadi atakapokutana na wadhamini, kisha ataelekea Wilayani Monduli atakakokuwa na mkutano wa hadhara pia.

Akizungumza na waandishi wa habari,kwenye ofisi za Chadema Mkoa, akiwa ameambatana na Viongozi wa Chama cha wananchi CUF wa Mkoa huo, Golugwa
amesema Lowassa anatarajiwa kushuka KIA majaira ya saa 3 tatu asubuhi na atakuwa ameongozana na viongozi wa Kitaifa wa Umoja wa Wananchi UKAWA.

Amesema wanatarajia kuwa na magari 75 yatakayobeba wafuasi wa Ukawa watakaopenda kwenda KIA kushuhudia historia ya aina yake ambayo yatondoka ofisi za Chadema Mkoa saa mbili asubuhi.

Pia amesema katika mkutano huo wanatarajia viongozi mbalimbali wa CCM wakiwemo wenyeviti wa serikali za mitaa, mabalozi na vigogo wengine watapokelewa rasmi katika mkutano huo wa hadhara.

Amesema kuhusu hali ya usalama ipo vizuri na watakuwa na ulinzi wa Polisi kwa kushirikiana na walinzi wa chama hicho ili kuhakikisha usalama na amani unatawala kwa kuw ana magri matano maalum ya wagonjwa.

Golugwa amesema pia kuna mmoja wa wafuasi amejitolea gari lake la kukusanyia takataka litakalopambwa kwa nembo za Chama na mgombea Urais wa UKAWA ambalo litatumika kutupia kadi za CCM ambazo wanatarajia zitakuwa nyingi kupitiliza.

Naye Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha Mjini, Derick Magoma, amesema kuwa kuanzia kesho, litapita gari maaluma la aina yake ambalo halipo Tanzania, lenye mziki mkubwa, sehemu ya kupumizikia na jukwaa, litaanza kupita mtaanai kutangaza ujuio wa Mheshimiwa Lowassa.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani