Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chadema yafunguka Lowassa kurejea jimbo la Monduli

Alhamisi , 16th Aug , 2018

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya jamii zikidai kuwa kamati kuu ya chama hicho imempitisha kuwania nafasi ya Ubunge jimbo la Monduli Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa.

Kamati Kuu ya (CHADEMA), imekutana katika kikao chake maalum jana Jumatano Agosti 15, 2018 kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali kuhusu chama hicho na taifa kwa ujumla.

Akizungumza na tovuti ya www.eatv.tv Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha, Amani Golugwa amesema kuwa taarifa za kuteuliwa Lowassa hazina ukweli wowote kwani kufanya hivyo ni kumshusha hadhi Waziri Mkuu huyo mstaafu na kudai kuwa hadhi yake kwa sasa ni nafasi ya urais.

Hayo sio mapendekezo ya kamati kama wanavyosema na hizo ni taarifa za uzushi na zinafanywa na wapinzani wetu kutaka kutuchafua, hakuna mgombea aliyepitishwa na mapendekezo yote yaliyotolewa ni ya awali,” amesema Golugwa.

Akizungumzia uamuzi wa Fred Lowassa kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha wanaowania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge jimbo la Monduli, Golugwa amesema baada ya kushauriana, vikao vya uteuzi vilikubali kuondoa jina lake.

Fred ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, alichukua fomu ya kuwania ubunge jimbo hilo wiki iliyopita lakini jana aliomba kujiondoa kwakile alichodai kuwa bado muda wake muafaka licha ya kuonekana kuungwa mkono na wanachama wengi awali.

Baada ya kujiondoa, Chadema kimempitisha diwani wa kata ya Lepurko, Yonas Masiaya Laizer kuwania ubunge wa jimbo hilo, kufuatia aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Julius Kalanga, kuachana na Chadema na kuachia ubunge na kuhamia CCM, ambapo Kalanga ameshateuliwa na CCM kugombea tena jimbo hilo.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya