Silaha.
Taarifa hiyo imetolewa leo Agosti 13, 2020 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Mtatiro Kitinkwi, na kutaja jina la Jambazi huyo aliyeuawa kuwa ni Daniel Jacksoni, ambapo aliuawa baada ya kukaidi agizo la Polisi walilomtaka kujisalimisha.
"Baada ya Jambazi huyo kuwaona Askari alikimbia huku akirusha risasi hovyo na baada ya kurusha risasi hizo na alijeruhi raia wawili, na baadaye Askari walimtaka ajisalimishe lakini akakaidi, na wao hawakumchelewesha wakampiga risasi", amesema Kamanda Kitinkwi.
Aidha Jeshi hilo linashikilia Bunduki aina ya short gun 12 bore(pump action), yenye namba MV.97465X ambayo ilikuwa ikitumiwa na marehemu katika tukio hilo la ujambazi.