
Antonio Guterres
Bw. Guterres alipendekezwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kumrithi Ban Ki Moon
Akizungumza mara baada ya kuidhinishwa, Bw. Guterres ameshukuru jinsi mchakato wa kumpata Katibu Mkuu mpya ulivyokuwa wa wazi na uliotoa washindani mbalimbali wenye uwezo.
Ameahidi kutumikia nchi zote kwa usawa bila bila upendeleo
Antonio Guterres amewahi kuwa Waziri Mkuu wa Ureno na pia amehudumu kama Kamishna wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR kwa miaka kumi na anatarajiwa kuanza kuitumia nafasi hiyo Novemba Mosi mwakahuu, baada ya Ban Ki-moon kumaliza muda wake Oktoba 31.