Tundu Lissu, mgombea Urais kupitia CHADEMA.
Akizungumza katika kampeni hizo amewataka wananchi hao kufanya maamuzi sahihi katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28, mwaka huu ili kupata Rais mwenye kujali uhuru na kuleta maendeleo.
"Niwaombe wana Morogoro muwachague viongozi waliobaki na ambao watarudishwa kwenye rufaa muwapigie kura ili mpate maendeleo", amesema Lissu.
Mgombea huyo pia amefanya harambee ya kuchangia kampeni hizo, ambapo amedai kuwa ili kampeni ziendelee lazima wasaidiane, "Sijapigwa risasi tu, nimepigwa kiuchumi, nilikua Mbunge na mnajua ulipoishia sasa hii kampeni tunaimalizaje inabidi tusaidiane, mimi nawaombeni mtuchangie sioni aibu".