Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Hatuna wa kumlilia" - Tundu Lissu

Jumapili , 15th Jul , 2018

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho kutumia vizuri fursa ya uchaguzi mdogo wa marudio uliopangwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu kwa kupambana kiakili ili waweze kushinda chaguzi hiyo.

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu

Lissu ametoa kauli hiyo leo Julai 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalum wa kijamii na kusema uchaguzi huo wa marudio katika Jimbo la Buyungu Mkoani Kigoma na kata 77 Tanzania Bara ni fursa kwao kuendelea kupigania haki za wananchi na utawala bora.

"Hakuna uchaguzi mdogo, kila uchaguzi ni muhimu katika mazingira halisi ya sasa ya kisiasa. Uchaguzi wa marudio wowote ule una kuwa na ugumu wa kipekee, tutafanyiwa na tayari tunafanyiwa kila aina ya fujo na CCM na mawakala wake kwenye Tume ya Uchaguzi na vyombo vya dola", amesema Lissu.

Pamoja na hayo, Lissu ameendelea kwa kusema "wajibu wetu ni kupambana kwa akili na maarifa ya hali ya juu ili kuzishinda fujo hizo na kushinda chaguzi hizo. Najua ni kazi ngumu, haijawahi kuwa rahisi mahali popote. Hatuna mjomba au shangazi wa kutufanyia kazi hii, au wa kumlilia baadaye tusipoifanya vizuri. Ni jukumu letu pekee".

Kauli hiyo ya Tundu Lissu imekuja yakiwa yamepita masaa machache tangu dirisha la kuanza kupiga kampeni kufunguliwa kwa kuomba ridhaa ya wananchi katika maeneo ambayo yatakuwa yana uchaguzi nchini Tanzania ifikapo Agosti 12 mwaka 2018.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita