Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jokate aipokea Namthamini, wanafunzi wanufaika

Jumamosi , 14th Dec , 2019

Zoezi la ugawaji wa pedi kwa wanafunzi wa kike katika shule mbalimbali nchini kupitia kampeni ya Namthamini, limeendelea katika mkoa wa Pwani, ambapo shule mbili za wilaya ya Kisarawe zimenufaika na kampeni hiyo.

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo (katikati) akipokea taulo za kike. Kushoto ni Mtangazaji TBway na kulia ni Deogratius Kithama.

Shule hizo ni Kibuta Sekondari ambayo ilipatiwa jumla ya pakiti 804 kwaajili ya wanafunzi 80 na watatumia kwa zaidi ya mwaka mmoja, hivyo kuwa na uhakika wa kutokosa masomo kwa changamoto ya kukosa pedi wakati wa hedhi.

Shule ya pili ni Maneromango Sekondari ambayo ilipatiwa jumla ya pakiti 1086 kwaajili ya 108, ambayo pia watakuwa na uhakika wa kuwa na taulo za kike kwa mwaka mzima.

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo, alishiriki kupokea taulo hizo katika shule zote akiwa ameambatana na timu ya East Africa Television na East Africa Radio.

Baada ya kupokea taulo hizo Mh Jokate aliwasihi wanafunzi kuona kama ni nafasi ya kujituma kwenye masomo ili kuwapa motisha watu waliochangia kuweza kuwasaidia tena.

'East Africa TV na East Africa Radio ni kampuni kubwa sana, wameacha kazi zao kwaajili ya kuja kuwathamini nyie, kwahiyo mnatakiwa muwalipe kwa kujituma na kufanya vizuri kwenye masomo yenu ili warudi tena', alisema Jokate.

Aidha Jokate aliishukuru East Africa Television na East Africa Radio kwa kuweka wazi kuwa zimemsaidia katika kampeni yake ya Tokomeza Zero Kisarawe kwa kutoa pedi hivyo kupunguza tatizo la utoro kwa wanafunzi wa kike wanapokuwa katika hedhi.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja