Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jumuiya yakanusha uvumi wa mgomo Kariakoo

Alhamisi , 17th Mar , 2016

Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini Tanzania JWT imekanusha uvumi uliozagaa mapema leo asubuhi kuwa wafanyabiashara katika eneo la Kariakoo wamegoma kufungua maduka.

Mandhari katika eneo la biashara la Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa uvumi huo, chanzo cha mgomo huo ni hatua ya wafanyabiashara kupinga ukaguzi unaofanywa na mamlaka ya mapato kwa kushirikiana na jeshi la polisi, wa kukagua wafanyabiashara wasiotoa risiti kwa bidhaa wanazoziuza.

Msemaji wa Jumuiya hiyo Bw. Steven Chamle ameiambia EATV kuwa biashara katika eneo la Kariakoo zimeendelea kama kawaida na kwamba kilichosababisha baadhi ya maduka kuchelewa kufunguliwa ni mkutano ambapo maofisa wa TRA walikutana na wafanyabiashara hao kwa lengo la kutoa ufafanuzi juu ya operesheni hiyo.

"Taarifa za mgomo sio za kweli bali kilichotokea ni mkutano ambapo idadi kubwa ya wamiliki na wauzaji wa maduka walihudhuria, mkutano ulioitishwa na Mamlaka ya Mapato mkoa wa Ilala kwa lengo la kutoa elimu juu ya zoezi linaloendelea la kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa risiti," alisema Chamle.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni rasmi na linaungwa mkono na Jumuiya hiyo kwani kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa sio watiifu kwa kutotoa risiti kwa mauzo wanayoyafanya.

Ameongeza "Sheria ya matumizi ya mashine za EFD inahusisha wafanyabiashara laki mbili tu kati ya takribani wafanyabiashara zaidi ya milioni mbili waliopo nchini hivi sasa na kwamba risiti za kuandika kwa mkono bado zinatumika kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao hawapo kwenye mfumo wa mashine za EFD,"

Aidha, msemaji huyo wa jumuiya ya wafanyabiashara amesema wao kama jumuiya wanaunga mkono operesheni hiyo na kamwe hawapo tayari kutetea wafanyabiashara wasiotoa risiti kwani kitendo hicho kinalenga kuinyima serikali mapato na hivyo kukwamisha shughuli za maendeleo.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea