Tukio hilo limetajwa kutokea alfajiri ya kuamkia leo Januari 13, 2020, baada ya magaidi hao kudaiwa kuvamia Shule hiyo.
Kwa mujibu wa Mwakilishi wa EATV kutoka nchini Kenya, amesema magaidi hao pia wamezima mawasiliano kwenye Mji huo wa Garissa, kwa kuharibu mnara wa simu wa kampuni ya Safaricom.
#HABARI Magaidi wanaoshukiwa kuwa Wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab wamevamia Shule ya Kamuthe Resource Center Mjini Garissa nchini Kenya, na kuwaua watu watatu, ambao wanadaiwa kuwa ni waalimu.
Aidha wameharibu mnara wa mawasiliano wa Kampuni ya Safaricom.
— East Africa TV (@eastafricatv) January 13, 2020
Tutaendelea kukuletea taarifa kila wakati kuhusiana tukio hilo.