Jumamosi , 18th Feb , 2023

Wanafunzi kote nchini Uganda  ambao watahitimu kujiunga na elimu ya A-Level, sasa watatakiwa kusoma kwa hadi miaka mitano, ikiwa serikali itaidhinisha mtaala mpya wa A-Level .

Awali, wanafunzi wamekuwa wakisoma Senior Five na Six katika kipindi cha miaka miwili kabla ya kujiunga na vyuo vikuu.

Naibu mkurugenzi wa mapitio ya mitaala na uendelezaji wa vifaa vya kufundishia katika Kituo cha Taifa cha Maendeleo ya Mitaala (NCDC), Bi Bernadette Nambi, alisema sehemu ya miaka mitano ni kumwezesha mwanafunzi ambaye hataweza kumaliza A-Level ndani ya miaka miwili kufanya mitihani yote  atakayofeli.

Pia Wanafunzi watakaofeli mitihani ya Uganda Advanced Certificate of Education (UACE) sasa watatakiwa kurudia somo lililofeli tu. Awali, ikiwa mwanafunzi atashindwa kufikia kanuni mbili kupita, atatakiwa kurudia mtihani mzima.