
Charles Mwijage
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage amesema hayo leo wakati wa siku ya mwisho ya mkutano wa kimataifa wa kilimo cha kibiashara, uliokuwa unaangalia upatikanaji wa mbolea barani Afrika na kufanyika jijini Dar es Salaam ambapo Tanzania ndio mwenyeji wa mkutano huo.
Mkutano huo umehusisha wasambazaji wa teknolojia mbalimbali za kilimo ikiwemo kampuni inayojihusisha na teknolojia ya uchambuzi wa sayansi ya udongo ambapo mkurugenzi wake Dkt. Edmund Matafu ameeleza uhusiano wa utengenezaji wa mbolea inayoendana na mahitaji ya udongo wa eneo husika.