
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana, akiagana na wananchi Ngorongoro
Wananchi hao ni wale waliokuwa wakiishi ndani ya eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ambao wameamua kuhama kwa hiari yao kuelekea Kijiji cha Msomera ili kupisha shughuli za uhifadhi.
Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana amewaaga wananchi hao akiwa na viongozi wa kamati ya amani na maridhiano nchini inayoundwa na viongozi wa dini pamoja na uongozi wa mkoa wa Arusha na kuwahakikishia kuwa serikali chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, imewaandalia mazingira mazuri na salama katika Kijiji cha Msomera.