Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kura ya maoni ifanyike baada ya uchaguzi

Alhamisi , 16th Apr , 2015

Wakazi wa wilaya ya Muheza wameishauri Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuahirisha zoezi la kuipigia kura Katiba Inayopendekezwa na badala yake isubiri hadi uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge ufanyike.

Katiba Inayopendekezwa.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara ulioitishwa kituo cha sheria na haki za binadamu kwa kushirikiana na tume ya taifa ya uchaguzi wakazi hao wamesema mapendekezo mengi waliyowasilisha katika rasimu ya kwanza ya katiba kwa mwenyekiti wa tume hiyo jaji Joseph Sinde Warioba yamepunguzwa hivyo ni lazima tume ijipange upya ili kuleta Demokrasia ya kweli nchini.

Kwa upande wake mwenyekiti wa wazee wa wilaya ya Muheza akielezea suala ya uhesabuji wa kura mara baada ya ya siku ya upigaji kura kufika, ameiomba tume ya taifa kufanya mabadiliko kwa waratibu wa uchaguzi ambao ni wakurugenzi wa halmashauri katika mchakato huo na badala yake watafutwe watu wa makundi tofauti yenye heshma kwa sababu watakosa imani ya kupata takwimu sahihi za waliopiga kura ya hapana na ndio.

Kufuatia hatua hiyo mratibu wa kampeni ya utoaji elimu kwa wananchi kuhusu Katiba Pendekezwa wa kituo cha sheria na haki za binadamu mkoa wa Tanga Bwana Stanley Gumbo amewataka wananchi kuzingatia elimu ya katiba zoezi hilo la kitaifa lengo lake ni kutaka wananchi wakubali kwa ridhaa yao ili kupata Katiba mpya.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja