Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

LHRC inafikiria uwezekano wa kupinga kura ya maoni

Jumanne , 21st Oct , 2014

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania – LHRC, pamoja na wadau mbalimbali wa mchakato wa katiba, wanajadili uwezekano wa kuchukua hatua za kisheria kuzuia zoezi la kura ya maoni kuhusu katiba mpya ambayo imepangwa kufanyika mwakani.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC) Dkt Hellen Kijo-Bisimba.

Akizungumza katika mahojiano na East Afrika Radio ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mkuu wa kituo hicho Dkt. Hellen Kijo-Bisimba, amesema kituo hicho hakioni mantiki ya kuharakishwa kwa kura ya maoni, kwani hadi kufikia Machi mwakani tume ya taifa ya uchaguzi NEC itakuwa haijakamilisha uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Kauli ya Dkt Kijo-Bisimba inafuatia kauli ya mwanasheria mkuu wa serikali Jaji Frederick Werema kuwa serikali inakamilisha taratibu za maandalizi ya kura hiyo kufanyika mwezi Machi mwakani.

Kwa mujibu wa Dkt Bisimba ni kipindi kifupi kutoka sasa hadi mwakani na kwamba idadi kubwa ya Watanzania hawajaandaliwa kushiriki zoezi hilo na kwamba iwapo litafanywa kwa kulazimisha kama ambavyo serikali inafanya sasa, kuna kila dalili kuwa katiha itakayopatikana haitakuwa bora kwani itakuwa imekosa ridhaa ya umma mkubwa wa Watanzania.

Aidha, Dkt Bisimba amesema harakati za kutaka kuharakishwa kwa kura ya maoni zilionekana mapema tangu siku Bunge Maalumu la Katiba lilipopitisha katiba inayopendekezwa, na kwamba ni vema serikali ikasitisha mchakato wa kutafuta katiba mpya hadi baada ya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge mwakani kama ilivyopendekezwa hivi karibuni katika mkutano wa kituo cha demokrasia TCD na kukubaliwa na vyama vyote vyenye uwakilishi bungeni.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala