Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

LHRC nayo yataka mchakato wa katiba usitishwe

Alhamisi , 7th Aug , 2014

Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC kimesema ni vyema Bunge Maalumu la Katiba likasitisha vikao vyake kutokana na kufanyika mabadiliko ya kanuni ambayo yatapelekea kupatikana kwa Katiba ambayo haina ridhaa ya wananchi.

Mkurugenzi mkuu wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Dkt Hellen Kijo-Bisimba.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa kituo hicho Dk. Hellen Kijo-Bisimba amesema kumekuwepo kwa kauli za baadhi ya viongozi wa serikali pamoja na wajumbe wa bunge maalumu, zinazoashiria mwelekeo mbaya wa kukiuka misingi ya kidemokrasia na utawala wa kisheria.

Aidha, Dk. Bisimba ameongeza kuwa kituo hicho kimesikitishwa na kupinga vikali kauli ya Mweyekiti wa Bunge la Katiba kutoa maelekezo kwa serikali ya Tanzania kupiga marufuku vyombo vya habari kutangaza midahalo inayohusu Katiba ambapo amesema matamko hayo yana lengo la kuwazuia watanzania kupata habari na taarifa juu ya mwenendo wa uboreshaji wa maoni yao yaliyopo kwenye rasimu na kujua hatma ya mchakato wa Katiba mpya.

Aidha katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Mkoani Arusha inawashikili kwa mahojiano wanne baada ya kubainika kuwa na uhusiano ya karibu na baadhi ya watuhumiwa wa kesi za ugaidi ambao kesi yao imeanza kusikilizwa jijini humo.

Akizungumza leo ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha SACP Liberatus Sabas, amesema watu hao wamekamatwa baada ya kufanyiwa upekuzi nyumbani kuwa ni Adam Mussa anayejulikana jina maarufu Pakasi, mkazi wa Siwandeti, Wilayani Arumeru na kukutwa bunduki ya kienyeji ikiwa na risasi 38 pamoja na bunduki aina ya Shortgun.

Kamanda Sabas mesema pia wanashikilia watu wengine watatu na baada ya kuwahoji wamebaini wana mahusiano ya karibu na watuhumiwa wa ugaidi wa kulipua mabomu na kumwagia watu tindikali, ambao wapo mahakamani.

Kamanda Sabas amesema mara baada ya uchunguzi kukamilika watuhumiwa huo watatu watafikishwa mahakamani, kujibu shitaka linalowakabili ambapo Oparesheni ya kuwakamata watuhumiwa zaidi wa matukio hayo inaendelea.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala