Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

LHRC yawataka viongozi waheshimu katiba

Alhamisi , 19th Mar , 2015

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania-LHRC kimewataka viongozi waheshimu Katiba na kuitaka sekretarieti ya maadili ya viongozi kusimamia maadili ya viongozi licha ya Katiba mpya kukosa vipengele muhimu ikiwemo kile kinachohusu maadili.

Mkurugenzi wa Utetezi wa LHRC Bw Harold Sungusia (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa uwezeshaji Bi. Emelda Urio (katikati).

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa uwezeshaji wa (LHRC) Bi. Emelda Urio amesema Katiba inayopendekezwa ina mapungufu mengi na kuwataka wananchi waweze kuisoma Katiba hiyo na kuwataka kuwa makini katika kutoa maamuzi ya upigaji kura kwa kuzingatia mambo muhimu yanayohusu utetezi wa haki zao.

Aidha, Bi Urio amewataka waandishi wa habari nchini kutumia nafasi zao katika kutoa elimu ya kutosha kuhusu masuala ya Katiba iliyopendekezwa na kutaka kuwepo na utekelezaji wa sheria ya maadili ya viongozi ya umma ikiwemo kuwajibishwa kutokana na kauli wanazotoa kwa umma.

Hata hivyo amesema viongozi wamekuwa wakiwarubuni wananchi wakati wa kuomba kura na pindi wanapopatiwa nafasi za uongozi husahau kutimiza ahadi alizotoa na hivyo katiba ya sasa inashindwa kutoa makali kwa wananchi kuwawajibisha viongozi hao.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Utetezi wa LHRC Bw Harold Sungusia amesema kumekuwepo na mkanganyiko katika utoaji wa adhabu na tume ya maadili kutokana na kuwepo kwa muingiliano baina yake na upande wa mahakama.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala