Maandalizi kwenye uwanja wa Uhuru ambapo atazikwa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Uhuru Temeke Jijini Dar Es Salaam amesema
"Tunashukuru sana kwa mapenzi yenu makubwa kwa viongozi wetu, naamini tutafika kwa wingi na wasioweza kupata nafasi uwanjani tunaomba mkae barabarani tutawapatia ratiba ni njia ipi ambayo mwili utapita hadi kufika hapa ili wote mmpate fursa ya kumuaga huko mlipo" Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Abubakari Kunenge
"Tunafanya taratibu kujua ni njia gani ambayo atapita pamoja na taratibu zingine ambazo zinafanywa katika ngazi ya Taifa kulingana na itifaki na niwahakikishie wananchi wa Mkoa wa Dar Es Salaam hali ya usalama ni nzuri na tumejipanga vizuri kwa hiyo tusiwe na wasiwasi tujitokeze kwa wingi na kuaga ni kuanzia asubuhi hadi jioni" ameongeza
Zaidi tazama kwenye video hapo chini.