
Baahi ya mabinti waliokatisha masomo baada ya kupata ujauzito mkoani Simiyu
Akizungumza wakati wa ufungaji mafunzo ya ujasiriamali kwa mabinti hao waliopata ujauzito wangali masomoni yaliyowezeshwa na Shirika la Restless Development, Meneja wa SIDO mkoa wa Simiyu, Athanas Moshi, amesema wameamua kutoa vyerehani hivyo kwa mabinti hao ili kuwa mwanga wa kiuchumi katika maisha yao na watoto wao.
Kwa upande wao, mabinti hao kupitia risala lao wamesema msaada huo wa vyerehani waliopewa na Shirika la SIDO watautumia vizuri katika suala zima la uzalishaji mali, ingawaje wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji.