Jumanne , 19th Mar , 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Hassan Abeid Mwang’ombe kuwa Posta Masta Mkuu.

Rais Magufuli

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Bw. Mwang’ombe umeanza tarehe 12 Machi, 2019.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Mwang’ombe alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Taarifa rasmi kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ni kama inayoonekana hapo chini.