Tundu lissu
Maamuzi ya kesi hiyo yametolewa leo Septemba 9, 2019 na Jaji Sirillius Matupa na kudai kwamba kesi hiyo ni ya kikatiba hivyo inapaswa kufunguliwa kwa mfumo wa kesi ya uchaguzi na si kwa mfumo ambao alikuwa ameutumia, huku pia akieleza kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kutengua ubunge wa Mbunge Julius Mtaturu aliyeteuliwa hivi karibuni.
Kesi hiyo namba 18 ya mwaka 2019, Lissu aliiomba Mahakama kibali cha kufungua shauri la kupinga taarifa ya Spika wa Bunge Job Ndugai ya kukoma ubunge wake, ambapo Mahakama imetupilia shauri hilo.
Kwa upande wa waleta maombi katika kesi hiyo, wameahidi kwamba watajipanga upya ili kufungua kesi ya uchaguzi na hatimaye kuipata haki yao. Hadi sasa Mbunge mteule wa CCM Julius Mtaturu, ataendelea kuwa Mbunge wa Singida Mashariki.