
LUKU
Utekelezaji wa sheria hiyo mpya ya kodi utafanyika kwa usimamizi wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), na TANESCO ambapo viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa jengo la kawaida kutoka 10,000 iliyokuwa ikitozwa hapo awali na shilingi 60,000 kwa kila sakafu moja ya ghorofa kutoka 50,000 ya awali.
Taarifa ya Kamishna Mkuu wa TRA Alphayo Kitada imesema utaratibu wa makato ya kodi ya jengo kwa mfumo huo, imekuja kufuatia marekebisho ya sheria ya kodi ya mamlaka ya serikali za mitaa iliyopitishwa na BUnge la Bajeti mwaka 2021, ambapo viwango vya kodi vimebadilishwa.