Ijumaa , 28th Aug , 2020

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Robert Boaz na DPP Biswalo Mganga, wamewasili kwenye Kisiwa cha Ukara, Ukerewe, kwa lengo la kufanya uchunguzi ili kuwabaini wanaotenda uhalifu uliopelekea mauaji ya watu wawili kisiwani hapo na kufanya wananchi kuishi kwa hofu.

DPP Biswalo Mganga

Hatua hiyo imekuja kufuatia kushamiri kwa vitendo vya uhalifu katika kisiwa cha Ukara kilichopo wilayani Ukerewe mkoani Mwanza hali iliyopelekea wakazi wa kisiwa hicho kuishi kwa wasiwasi.

Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini DCI kamishna Robert Boaz na Mkurugenzi wa mashtaka nchini DPP Biswalo Mganga wamefika katika kijiji cha Bukungu kilichopo katika kisiwa hicho na kuwatoa hofu wakazi hao.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Robert Boaz

Viongozi hao wameambatana na mwenyeji wao RPC wa Mwanza Muliro Jumanne ambaye naye ameahidi kuwa mauaji hayo yatakomeshwa.

Zaidi tazama Video hapo chini