Mbatia ametoa kauli hiyo baada ya kumalizika kwa ibada ya misa takatifu ya Jubilee ya fedha ya miaka 25 ya Padri Thomas Salekio Kessy, iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Yohana mkoani Kilimanjaro.
Mbatia amesema kuwa, "majuzi nilisikia na kusoma baadhi ya maandiko kwamba watu Wanamibia wao wanasema mwanafunzi anayetoka Tanzania, amemaliza kidato cha sita akienda kwao, kupata Chuo Kikuu kule ni shida, kwa sababu Namibia wao mfumo wao ni mgumu, wao elimu zao wanamalizia kidato cha nne.
"Unajiuliza silabasi zetu zimeundwa namna gani, nawashauri wakuu wa nchi wanachama ni vizuri tukawa na sera moja ya SADC katika masuala ya elimu,” amesema Mbatia.
Mwaka huu Tanzania imekuwa mwenyeji wa mkutano wa 39 wa SADC, ikiwa imepita miaka 16, tangu mkutano kama huo kufanyika kwa mara ya mwisho mwaka 2003, chini ya utawala wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.