Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Singida kupitia CHADEMA, Jesca Kishoa
Mbunge Kishoa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na www.eatv.tv iliyotaka kufahamu juu ya changamoto anazokutana nazo kama Mbunge mwanamke ndani siasa za Tanzania.
Akizungumza na www.eatv.tv Mbunge huyo amesema, "mwaka 2015 niligombea Ubunge nikiwa na ujauzito wa miezi tisa na nilijifungua kipindi cha kampeni lakini niligeuza kuwa fursa, kwa sababu nilipata huruma ya watu na chama changu."
"Changamoto nyingine wanayokutana nayo wanawake ni rushwa ya ngono kwenye siasa wengine wanaamini ili upate nafasi ya siasa lazima utoe rushwa ya ngono japo ina ukweli na ina uongo." ameongeza kishoa.
Mapema hivi karibuni Mbunge huyo alisema licha ya yeye kuwa chama tofauti na mume wake ambaye ni David Kafulila, lakini wamewekeana utaratibu kila mtu kuheshimu itikadi ya mwenzake.