Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mch. Msigwa,afikishwa mahakamani mkoani Iringa

Alhamisi , 8th Oct , 2015

Mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia (CHADEMA), Mch. Peter Msigwa na wafuasi wengine watatu wa chama hicho wamefikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka yanayohusiana na uvunjifu wa amani pamoja na kuwashambulia askari wa jeshi la polisi.

Mgombea Ubunge jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kutoka Mahakamani Jana

Mchungaji Msigwa na wenzake watatu wamefikishwa mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa David Ngunyale na kusomewa mashitaka manne yakufunga barabara na kusababisha uvunjifu wa amani,kuharibu gari ya jeshi la polisi pamoja na kuwashambulia na kuwajeruhi askari polisi wawili akiwemo kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoani iringa.

Washitakiwa hao wanne ni sehemu tu ya watuhumiwa kumi wanaotuhumiwa kwa vurugu hizo zilizotokea siku ya tarehe 28 mwezi septemba, ambapo awali taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi iliwatuhumu wafuasi wa chadema kwa kufunga barabara na kuwafanyia vurugu wafuasi wa Chama cha Mapinduzi waliokuwa wametokea kwenye mkutano wa mgombea urais kupitia chama chao uliofanyika kwenye uwanja wa Samora

Washitakiwa wote wameachiwa kwa dhamana mpaka kesi yao itakapotajwa tena Novemba 2 mwaka huu ambapo mgombea ubunge wa jimbo la iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amesema pamoja na mashitaka hayo wanachadema hawapaswi kukata tamaa ya kufanya kampeni za amani ili kuhakikisha wanashinda.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao