Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mgombea wa CHADEMA ashambuliwa

Jumapili , 12th Aug , 2018

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limesema limefungua jalada la uchunguzi la tukio la vurugu katika uchaguzi mdogo wa marudio kata ya Kaloleni jijini Arusha baada ya watu wawili kudaiwa kuchomwa visu na kikundi cha vijana wa 'Green guard' kutoka CCM. 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi

Akizungumza na www.eatv.tv Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi amesema walipigiwa simu na Mbunge wa Arusha wa Mjini (CHADEMA), Godbless Lema kuwa mgombea wao Boniface Kimario amevamiwa na kuamuru askari waliokuwa karibu na maeno hayo kuenda kutuliza hali ya usalama.

"Asubuhi kulitokea ushabiki wa kisiasa kati ya makundi mawili ambayo ni ndio sasa hivi tunachunguza, na ushabiki huo ndio ulisababisha huyo mgombea wa CHADEMA kupigana na watu wengine. Kutokana na maelezo yake amesema akiwaona hao watu anawatambua hivyo tunamsubiri amalize kutibiwa ili aje atuambie ni wakina nani hasa. Lakini yeye hakuchomwa kisu", amesema Kamanda Ng'azi.

Pamoja na hayo, Kamanda Ng'azi ameendelea kwa kusema "isipokuwa kuna mwanachama mmoja wa CCM alijeruhiwa na kitu chenye ncha kali juu ya kiwiko chake cha mkono wake wa kulia. Tumeshamkamata mtuhumiwa mmoja ambaye amemjeruhi mwanachama wa CCM"

Mbali na hilo, Kamanda Ng'azi amesema hali ya uchaguzi inaendelea vizuri katika mkoani mzima wa Arusha hadi hivi sasa ambao una jumla ya kata tatu ambazo ni Kaloleni, Daraja Mbili pamoja na Osinyayo.

Msilikize hapa chini, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi akisimuliza zaidi juu ya tukio hilo.

 

HABARI ZAIDI

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita