Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkuu wa Wilaya avunjiwa nyumba

Ijumaa , 19th Apr , 2019

Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara limewakamata watuhumiwa 21, wanaojihusisha na matukio ya uhalifu ikiwemo uvunjaji wa nyumba na wizi wa pikipiki, ambapo miongoni mwa wahanga wa matukio hayo yumo Mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda ambaye ameibiwa vitu vyake vya ndani.

Kamanda wa Polisi Mkoani wa Mtwara, Blasius Chatanda-ACP,

Kamanda wa Polisi Mkoani wa Mtwara, Blasius Chatanda-ACP, amesema operesheni hiyo imeanza 01 January 2019 hadi 18 April 2019 ambapo ndani ya kipindi hicho wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 21 wanaojihusisha na matukio ya uhalifu pamoja na mali mbalimbali.

"Katika operesheni inayoendelea Mtwara tumewakamata watuhumiwa 21, pia tumekamata mali mbalimbali zidhaniwazo kuwa za wizi ikiwemo TV 12, Deki 3, Sub wofer 2, kompyuta 7, Solar panel 11 ,mitungi ya gesi 17, pikipiki 7, bajaji moja na zana za uvuvi haramu ikiwemo viroba vitatu vyenye unga unaodhaniwa ni sumu" amesema Kamanda Chatanda.

Aidha, Kamanda Chatanda amesema miongoni mwa wahanga wa uhalifu huo ni Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Evod Mmanda ambaye ameibiwa vifaa vya ndani.

"Mkuu wa wilaya ya Mtwara ni miongoni mwa wahanga wa huu uhalifu tulioubaini wakati wa operesheni, yeye ameibiwa vifaa vya ndani ikiwemo TV(Flat Screen)usiku wa 17/04/2019, hawakufanikiwa kuchukua vingine kwakuwa wahalifu hao baadae walikurupushwa ila waliohusika na tukio hili tayari tunao" amesema.

Ameongeza kwamba, "tunawaomba walioibiwa katika matukio mbalimbali, wafike kituo kikuu cha polisi kati mjini Mtwara ili waweze kuzitambua mali zao"

Kamanda Chatanda amesema licha ya mkuu wa wilaya kuibiwa, katika Kompyuta zilizokamatwa pia zimo zilizoibiwa kwenye ofisi za halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani.

"Miongoni mwa Kompyuta zilizoibiwa pia zimo ambazo zimeibiwa kwenye Ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya  Mtwara Mikindani, tunajiuliza huyu aliyeiba alikuwa na lengo la kuvitumia tu au alikuwa anataka baadhi ya taarifa za ofisi. Watumishi wawili wa Halmashuri wanaotuhumiwa tumewashikilia na tunaendelea na uchunguzi",  amesema Chatanda.

HABARI ZAIDI

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita