Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mtwara ndio muhimili mpya wa Uchumi Tanzania-JK

Jumatatu , 10th Aug , 2015

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amewataka wanasiasa mkoani Mtwara kuacha tabia za kuwapotosha wananchi kwa kuwaeleza mambo yasiyo na ukweli, na badala yake wawaeleze juu ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa.

Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa Msanga Mkuu-Mtwara vijijini waliofika kwenye uzinduzi wa kivuko cha MV Mafanikio

Akizungumza katika hotuba fupi aliyoitoa wakati wa kuweka jiwe la msingi katika jengo la Benki Kuu ya Tanzania (B.O.T) tawi la Mtwara, alisema Mtwara ndio muhimili mpya wa uchumi wa Tanzania kutokana na kuwa na rasilimali nyingi zinazotoa fursa za uwekezaji.

Kwa upande wake, Gavana wa B.O.T, Prof. Benno Ndulu, amesema Tanzania imepiga hatua katika matumizi ya teknolojia ya huduma za simu za mkononi za kibenki zenye gharama nafuu na kufanikiwa kuwa katika nafasi ya 10 duniani kwa nchi zinazoongoza kwa teknolojia hiyo huku ikiwa nafasi ya kwanza barani Afrika.

Wakati huo huo rais Kikwete, amezindua kivuko cha Mv Mafanikio kinachosafirisha abiria kutoka Mtwara-Msangamkuu, chenye uwezo wa kubeba abiria 100 na magari sita kwa wakati mmoja.

Akiwahutubia wakazi wa kata ya Msangamkuu, Rais Kikwete amewaahidi wananchi wa kata hiyo kuwakamilishia mradi wa maji ambao unatekelezwa huku ukikabiliwa na uhaba wa fedha kiasi cha shilingi milioni 400.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais, waziri wa ujenzi na mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. John Magufuli, ameagiza wanafunzi wa ngazi zote kusafiri bure kwa kutumia kivuko hicho ambacho ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 3.5

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea