Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Muimbaji Nyota azungumzia kifo cha Mzee Njenje

Jumapili , 24th Mei , 2020

Muimbaji wa Bendi ya Kilimanjaro, Nyota Waziri, amezungumzia kifo cha Mkongwe wa Bendi hiyo Mabrouk Omar maarufu kama Mzee Njenje, na kusema kuwa alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya muda mrefu yaliyosababishwa na uzee.

Muimbaji wa Bendi ya Kilimanjaro, Nyota Waziri na kulia ni Mzee Njenje.

Hayo ameyabainisha leo Mei 24, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, ambapo pia tulizungumza na ndugu wa karibu wa Mzee Njenje na kwa pamoja walikuwa na haya ya kusema.

"Ni kweli amefariki leo Alfajiri na alikuwa anaumwa kwa muda mrefu, na juzi hapa alianza kuumwa tena, mazishi ni leo anazikwa Makaburi ya Kisutu" amesema Nyota Waziri.

Kwa upande wake ndugu wa karibu wa Mzee Njenje aliyejitambulisha kwa jina la Naima George amesema kuwa, "Alikuwa anaumwa na hali imebadilika tangu juzi, tulimpeleka Hospitali akapata huduma ya kwanza, Daktari akashauri apumzishwe kwa siku tatu, bahati mbaya leo Mungu kampenda zaidi, alipa stroke na ilimjia kama mara mbili hivi, lakini pia alikuwa anasumbuliwa na macho, figo na presha pia, ana watoto wawili na mke mmoja".

Mzee Njenje amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 73 na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na mara baada ya kuswaliwa utapelekwa moja kwa moja katika makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi hii leo.

Ikumbukwe kuwa Mzee Njenje, alitamba na nyimbo kama, Kinyaunyau, Kachiri, Ndembere pamoja na Boko.
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi