Kiongo Mkuu wa ACT Wazalendo, akiwa mahakani.
Kesi hiyo namba 327 ya mwaka 2018, ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa, ambapo ulitokea mvutano wa Mawakili juu ya Hakimu kupokea ama kutokupokea ushahidi wa CD ili kusikia maneno aliyoyaongea Mbunge Zitto, wakati wa mkutano wake na Waandishi wa Habari, hali iliyopelekea kesi hiyo kuahirishwa hadi Desemba 4, 2019.
Zitto anakabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi, anayodaiwa kuyatenda Oktoba 28, 2018, katika mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika makao makuu ya ofisi za chama hicho zilizopo Kijitonyama, Jijini Dar es Salaam.