
Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe
Taarifa ya mauaji hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe na kusema tukio hilo limetokea mtaa wa Majengo, Kata ya Kanyara, halmashauri ya mji Geita, ambapo mwanamke huyo aitwaye Anjela Anteli (43), alikutwa amenyongwa.
Kamanda Mwaibambe, amesema kuwa mtu wa kwanza kugundua alikuwa bodaboda ambaye aliagizwa kupeleka maziwa nyumbani hapo na alipofika akagonga mlango bila mafanikio.