Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mzee wa miaka 70 ahukumiwa miaka 90 jela

Alhamisi , 26th Mei , 2022

Mahakama ya wilaya ya Lindi, imemhukumu mkazi wa Kijiji cha Namkongo,Kata na Tarafa ya Mipingo, mkoani humo Salum Mtopa mwenye umri wa miaka 70 kifungo cha miaka 90 gerezani, baada ya kukutwa na hatia kwa makosa matatu, likiwemo kumiliki shamba linalohusika na kilimo cha bangi.

Nyundo ya Hakimu

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo,Maria Batraine, baada ya kuridhishwa pasipo shaka na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo,Hakimu Batraine alimuuliza mshtakiwa kama ana sababu za msingi itakayoishawishi Mahakama isimpe adhabu kali, aliomba isimpe adhabu kali kwa madai ni mkosaji wa mara ya kwanza,umri wake umeshakwenda,pia anayo familia  inayomtegemea mke na wajukuu watano.

"Mhe, Hakimu kama unavyoniona mimi sasa ni mzee na nina wajukuu wananitegemea,ukinipa adhabu kubwa watakosa huduma zangu," Aliomba Mtopa.

Baada ya utetezi huo,Hakimu alimuuliza mwendesha mashtaka, Mkaguzi John Ijumba, kama anazo kumbukumbu ya makosa ya zamani kwa mshitakiwa na kujibu hana, huku akiiomba Mahakama impe mshtakwa adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine walio na tabia ya aina hiyo.

Hakimu Batraine akitoa hukumu katika kesi hiyo ya Jinai Namba 46/2021,kupitia vifungu 11 (i)(b) na 11 (1) (a) kama vilivyofanyiwa marejeo 2019,alisema makosa aliyofanya mshitakiwa yapo kwa mujibu wa sheria, hivyo hana uwezo wa kubadilisha,na kumhukumu kosa la kwanza kukutwa na nangi kutumikia kifungo cha miaka 30 Jela.

Kosa la pili kushiriki kukutwa na mbegu kutumikia kifungo cha miaka (30),pa adhabu ya aina hiyo alipewa kwa kosa la tatu la kusafirisha bangi kutumikia gerezani kifungo cha miaka (30) na kufanya Jumla ya miaka kuwa 90 na kwa vile adhabu zinakwenda kwa pamoja mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka (30).

Aidha,mshitakiwa ameambiwa nafasi ya kukata rufaa ipo wazi kama atakuwa hakuridhishwa na hukumu iliyotolewa na Mahakama hiyo ya wilaya.

Mshtakiwa alifanya kosa hilo Julia 20, 2021, huko Namkongo baada ya kukutwa akiwa na jumla ya kilogram 151.99 za madawa ya kulevya aina ya bangi, kati ya hizo, kilogramu 132.94 ni mbegu, pia alikutwa akimiliki shamba la bangi lenye ukubwa wa ekari 5.54.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita