Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ndege za Tanzania kuwafuata kwao Wachina laki 1

Jumamosi , 17th Nov , 2018

Serikali imewahakikishia watalii nchini China kuwa, wataanza kufuatwa na ndege za shirika la Air Tanzania, na kuwaleta moja kwa koja nchini kwaajili ya masuala mbalimbali ikiwemo utalii na biashara.

Uwanja wa ndege wa Guangzhou

Hayo yameelezwa na Wizara ya Maliasiri na Utalii, kupitia kwa meneja mauzo na usambazaji wa Air Tanzania Edward Nkwambi na Mkurugenzi mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Devotha Mdachi ambao wamesema lengo la serikali ni kuongeza watalii na wafanyabiashara.

''Tumekuja na mawakala wa Utalii Tanzania hapa Beijing ambapo tuna ziara katika miji 6 na tunauhakika kuwa ifikapo mwezi Februari 2019 idadi ya watalii kutoka China wataongezeka kwani watakuwa na fursa ya kutumia ndege za Air Tanzania moja kwa moja kutokea hapa'', alisema Nkwabi.

Aidha ameongeza kuwa ndege mpya ya kisasa ya 'Dreamliner' itakuwa inafanya safari hizo kutoka Guangzhou hadi Dar es salaam jambo ambalo lazima liongeze idadi ya watalii na kuchocheza ukuaji wa uchumi kupitia biashara kwani China imeendelea kwenye sekta hiyo.

Kwa upande wake Devotha Mdachi amesema Bodi ya Utalii Tanzania inategemea kuona idadi ya watalii kutoka China ikiongezeka kutoka Elfu 30 hadi 60 kwa mwaka na laki moja ndani ya miaka miwili ijayo kutoka na urahisi wa usafiri utakaokuwepo.

Ndege ya Dreamliner ambayo ilinunuliwa na serikali, ina uwezo wa kubeba abiria 240 kwa wakati mmoja na pia ina uwezo wa kufanya safari za moja kwa moja za masafa marefu ikiwemo China na Marekani.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera