Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Ni dhambi kuchukua sifa isiyo yako"- Polepole

Ijumaa , 11th Jan , 2019

Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM amepinga suala la Mbunge wa Bunda Mjini kutambuliwa na kupewa sifa kwamba aliwatetea wafanyakazi juu ya mafao kwa kipinga hadharani kikokotoo kipya na badala yake itambuliwe serikali ya CCM chini ya Rais Magufuli.

Pichani, Kushoto ni Rais wa Tanzania, John Magufuli, (kulia) ni Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole katikati.

Akizungumza na www.eatv.tv, Polepole amesema kwamba aliyesimama na jambo la kikokotoo tangu mwanzo ni serikali ya CCM na aliyehitimisha jambo hilo ni Rais Magufuli mwenyewe.

Ameongeza kwamba Rais Magufuli baada ya kusikiliza maoni ya wawakilishi na baadhi ya viongozi wa wafanyakazi akaamua kufanya maamuzi ambapo pia aliweka utaratibu na utaratibu huo umeshaanza kufanya kazi.

"Ni dhambi kuchukua sifa ambayo si yakwako. Siyo kweli kwamba ni yeye, aliyesimama na jambo hili, tangu mwanzo ni serikali ya CCM na aliyehitimisha jambo hilo ni Rais Magufuli mwenyewe. Maoni na mitazo ilikuwa mingi, ni haki ya kila mtanzania kila mmoja ana uhuru wa maoni. CCM inaheshimu uhuru hatutashangaa kila mtu akiweka maoni hadharani.

Mwezi Novemba mwaka uliopita, Spika wa bunge alimsifu Mbunge wa Bunda Mjini (CHADEMA), Ester Bulaya, ambaye pia ni Waziri Kivuli Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), aliyeibua suala kutumika kwa kanuni mpya kwenye mafao ya wastaafu.

Bulaya aliwaambia waandishi wa habari kuwa, kikokotoo hicho kipya kilichotungwa na serikali ni kitanzi kwa wastaafu kwa kuwa hawatanufaika na fedha zao ambazo wamezitolea jasho kwa miaka mingi.

Baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi, Rais Magufuli alipokutana na viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), vyama shiriki, watendaji wakuu wa mifuko ya Hifadhi ya jamii ya PSSSF na NSSF na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) Desemba 28, aliagiza kikokotoo kilichokuwa kikitumika awali kieendelee katika kipindi cha mpito mpaka mwaka 2023.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi