Jumatatu , 24th Sep , 2018

Rais mstaafu wa awamu ya nne wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema alipotakiwa kuacha kuvaa viatu shuleni na mwalimu wake wa shule ya msingi ndio sababu iliyopelekea kukiita kitabu chake safari ya kutoka shule bila viatu hadi Urais.

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Rais Mstaafu Kikwete ameyasema hayo hivi karibuni wakati akizindua usomaji wa kwanza wa kitabu chake katika Chuo Kikuu cha Newyork kilichopo Marekani ambacho amekipa jina “The Journey of My Life From a Barefoot Schoolboy to President”.

Rais Kikwete amesema “Nilipata viatu (raba) kwa mara ya kwanza nilivyotoka jandoni ,nilikwenda navyo shule mwalimu akanambia kesho usije na viatu kila mtu hana viatu humu, kitu muhimu nachowashauri wazazi wawasaidie watoto wao kusoma, na watoto watimize wajibu wao wa kusoma".

Kitabu hicho kinatarajiwa kufanyiwa tafsiri ya kiswahili ikielezea maisha ya kiongozi huyo mstaafu ambae alishawahi kuiongoza Tanzania kama wa Rais wa awamu ya nne kuanzia mwaka 2005 hadi 2015 akiwa pia Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM).