Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Nimechapwa bakora hadharani mara 7’- RC Mbeya

Jumatatu , 21st Oct , 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya albert Chalamila, amesema na yeye alishawahi kucharazwa bakora hadharani, wakati akiwa anasoma elimu ya Sekondari na kudai kuwa bakora hizo ndiyo zilizomsaidia mpaka sasa amekuwa Mkuu wa Mkoa, pamoja na kushika nafasi zingine za uongozi kwenye siasa.

Chalamila ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na EATV / EA Radio Digital, kuhusiana na hatma ya wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Kiwanja, ambao aliwatimua kurudi nyumbani na kuwataka kulipa faini ya shilingi laki 2 kila mmoja, ambapo amesema mpaka sasa jumla ya wanafunzi 207 wameshalipa.
 

Mimi ni Mwalimu nimeshafundisha Shule za Sekondari 17, na Vyuo Vikuu kwa hiyo mimi ninatandika sana, nimeshawahi kuwa Mkuu wa Shule na baada ya hapo ndiyo nikaacha nikahamia kwenye masuala ya siasa."amesema Chalamila.

Aidha Chalamila ameongeza kuwa, "Kuhusu mimi kuchapwa hadharani nimeshachapwa sana wakati nikiwa nasoma tena nipiga karibia mara saba na nimechapwa kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo makosa ya kutofanya usafi, kuleta migomo na kusababisha migomo, na hata siku ya mwisho ya mtihani wangu wa form four nilipotoka kwenye mtihani wangu wa hesabu nilichapwa na Mwalimu wangu Robert".

Leo Jumatatu Mkuu huyo wa Mkoa, anatarajiwa kutoa hatma ya wanafunzi 56 wa Shule ya Sekondari Kiwanja , ambao aliwatimua Shuleni na kuwataka kulipa faini kwa tuhuma za kutishia kuchoma moto mabweni.

HABARI ZAIDI

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria