Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyalandu aivunja Idara ya Wanyamapori

Ijumaa , 11th Jul , 2014

Waziri wa maliasili na utalii nchini Tanzania Lazaro Nyalandu, ametangaza kuivunja idara ya wanyamapori na kuunda mamlaka ya wanyamapori, kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yake kiasi cha kusababisha matukio ya ujangili na uwindaji haramu.

Waziri wa Maliasili na Utalii nchini Tanzania, mhe. Lazaro Nyalandu.

Waziri Nyalandu ametangaza hayo leo jijini Dar es Salaam sambamba na kutangaza kufuta leseni za uwindaji na uendeshaji wa vitalu vyote vilivyotolewa kwa kampuni ya Green Miles Safaris ambayo hivi karibuni waziri kivuli wa maliasili na utalii Mchungaji Peter Msigwa alianika kile alichokiita ukiukwaji mkubwa wa sheria ya wanyamapori.

Kwa mujibu wa Waziri Nyalandu, majukumu yote yaliyokuwa chini ya idara ya wanyamapori yatakuwa chini ya mamlaka ya wanyamapori itakayoundwa hivi karibuni, mamlaka aliyosema itakuwa na mamlaka kamili ya kiuendeshaji na kusimamiwa moja kwa moja na wananchi.

Jumpili iliyopita, Waziri kivuli wa maliasili na utalii Mchungaji Peter Msigwa alionesha kwa waandishi wa habari mkanda wa video na kuanika kile alichookiita kuwa ni uozo na ukiukwaji mkubwa wa sheria ya wanyama pori unafanywa kupitia vitalu vya uwindaji.

Mchungaji Msigwa alifichua namna makampuni yaliyopewa leseni ya uwindaji ikiwemo ya Green miles Safaris Ltd, ilivyovunja sheria ya wanyamapori kwa kuwauwa wanyama wadogo, kufanya ukatili wakati wa kuwakamata na hata kukiuka sheria za kimataifa ambazo Tanzania kama nchi imeziridhia.

Aidha, Mchungaji Msigwa alimtaka waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu kuwawajibisha watendaji wote katika idara ya wanyamapori sambamba na kuchukua hatua kali dhidi ya kampuni ya Green Miles Safaris ikiwa pamoja na kuifutia kampuni hiyo leseni ya uwindaji.
…........................................

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa