Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

PAC chini ya mwenyekiti mpya yaanza na SUMA JKT

Jumanne , 18th Oct , 2016

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imemchagua Mhe. Naghenjwa Kaboyoka Mbunge wa Same Mashariki (Chadema) kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo.

Kamati ya PAC, katika kikao chake chini ya mwenyekiti mpya

Tangu kuundwa kwa Kamati hiyo ambayo kwa mujibu wa Kanuni za Bunge inatakiwa kuongozwa na Upinzani ilikuwa bado haijamchagua Mwenyekiti na hivyo ilikuwa chini ya Uongozi wa Makamu Mwenyekiti Mhe. Aeshi Hilaly (Mb).

Katika uchaguzi huo Mhe. Kaboyoka hakupigiwa kura badala yake alipendekezwa na Wajumbe wa Kamati hiyo ambapo wote waliridhia awe Mwenyekiti wao.

Kamati hiyo ilikutana katika kikao chake cha kwanza chini ya Mwenyekiti Mhe. Kaboyoka ambapo mara baada ya kufanya uchaguzi huo ilijadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu Hoja za Ukaguzi kwa Mashirika yaliyoko chini ya SUMA JKT.

Wajumbe wa Kamati hiyo walisema hesabu za mashirika hayo hazijazingatia sheria na utayarishaji wa hesabu na kwamba matumizi yao yamezidi bajeti iliyoidhinishwa.

Kamati hiyo ilitoa ushauri kwa SUMA JKT kuhakikisha wanaajiri wahasibu wenye ujuzi badala ya kuajiri watu ambao hawana ujuzi wa kuandaa taarifa za fedha.

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Michael Isamuhyo alikiri kuwepo kwa mapungufu hayo na kwamba kwa sasa Jeshi hilo limepeleka maombi Wizarani kuomba kutenganisha shughuli za SUMA na JKT.

Wakati huohuo , Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) jana ilipokea majumuisho ya shughuli za Kamati kwa kipindi cha kuanzia Agosti 15, 2016 hadi Septemba 2, 2016.

Aidha, Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa jana ilipokea maelezo kuhusu shughuli za Kamati katika kipindi cha Oktoba 17 haadi 30, 2016.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa