Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe
Taarifa hizo zilieleza kuwa BAWACHA wataendesha maandamano kutoka wilayani Chato kuelekea Dodoma, kuhusu kumpinga spika wa Bunge juu wabunge 19 wakuteuliwa ambao hawana chama.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe anasema hana taarifa yeyote kuhusu maandamano hayo hivyo kama wamepanga kufanya hivyo basi wafate taratibu.
Mwenyekiti wa BAWACHA mkoa wa Geita Hellena Thobias na mwenyekiti wa BAWACHA wilaya ya Chato, Husna Saidi wamesema wataendelea na msimamo wao jinsi walivyojipanga kufanya maandamano hayo kuelekea Dodoma.