Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Prof. Ndalichako atoa onyo kwa wasimamizi wa elimu

Jumatano , 27th Apr , 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako, amewatahadharisha kuwawajibisha maafisa elimu wa shule za msingi watakaoshindwa kusimamia elimu na kusababisha wanafunzi wamalize shule za msingi bila kujua kusoma na kuandika.

Waziri wa Elimu,Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako

Prof. Ndalichako amesema hayo Mjini Iringa katika mafunzo ya wakaguzi na wadhibiti wa ubora wa elimu mashuleni kutoka wilaya 31 kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Prof. Ndalichako amesema kuwa ni aibu kwa wanafunzi waliosoma miaka saba darasani hawajui kusoma na kuandika wakati Wakaguzi na Wasimamizi wa Elimu wapo katika maeneo husika na kuwataka wajitathimini kama wanatekeleza wajibu wao ipasavyo.

Waziri huyo pia amewataka wadhibiti hao wa elimu kufanya ukaguzi wa vitabu na vifaa vya kufundishia vikiwa na ubora unaokubalika huku akiahidi kuzingatia mahitaji ya walemavu katika shule za serikali.

Kwa upande wao walimu pamoja na wadhibiti hao wa elimu wameiomba serikali kushughulikia madai yao na kuboresha mazingira ya kufanyika kazi ikiwemo pamoja na fungu la kutosha na kuendeshea ukaguzi wa elimu.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao