Katika hotuba hiyo amezilaumu nchi za Magharibi kwa kuchochea vita na kuvizidisha, akisema Marekani na washirika wake wanatafuta nguvu isiyo na mipaka.
Katika tangazo pekee kubwa, alisema anasitisha ushiriki wa Urusi katika makubaliano makubwa ya kudhibiti silaha na Marekani. Hotuba hiyo imekuja kuelekea maadhimisho ya kwanza ya uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine siku ya Ijumaa.
Wakati hayo yakijiri Rais wa Marekani Joe Biden anatarajiwa kuweka wazi mtazamo wake kuhusu vita vya Ukraine kama vita vya demokrasia wakati wa hotuba yake baadaye Jumanne.
Atatoa hotuba yake katika mji mkuu wa Poland, Warsaw ikiwa ni siku moja baada ya ziara yake ya kushtukiza nchini Ukraine.



