Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Raia 7 wakigeni wakamatwa kwa wizi mitandaoni Dar

Jumamosi , 12th Sep , 2020

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa amesema jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata majambazi 9 wanaotapeli watu kwa njia ya mtandao miongoni mwao saba wakiwa ni raia wa Tanzania.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani.

Kamanda Mambosasa amesema kutokana uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo umewakamata na kuwa watachukuliwa hatua za kupelekwa Mahakamani na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria na na ametoa onyo kwa wale wote wanaondelea kufanya vitendo hivyo ikiwa ni pamoja na kuwaomba wananchi kutoa taarifa wanapobaini kuwepo kwa matukio kama hayo.

Amewataja watuhumiwa hao kutoka mataifa mbalimbali ya kigeni kwa tuhuma za kufanya uhalifu kwa njia mtandao (CYBER CRIME) na kuwataja Watuhumiwa hao kuwa ni ADEWALE NUREN OYEDES (34) Raia wa Nigeria ,IBRAHIM DARBEY (44) Raia wa Liberia CREAM MILTON ELIAS (38) Raia wa Liberia ,BASUBE DOMINIC (44), Raia wa DRC ,PRINCE TITO (46), Raia wa Liberia, SIBONGILE ARHUR (44), Raia wa Afrika Kusini. NA BALJIT SINGH (28), Raia wa India.

Aidha Mambosasa amesema kuwa jeshi hilo linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kujifanya maofisa usalama wa Taifa, Polisi na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ambao ni PATRICK TARIMO (32), Mkazi wa Mwenge, anajitambulisha kama afisa usalama wa Taifa. Na CASTORY WAMBURA (57), Mkazi wa Kibamba, anajitambulisha kama ofisa wa Polisi na kwamba watuhumiwa wote wawili wamekuwa wakitapeli raia wema kwa kujifanya waajiriwa wa Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Polisi.

“Mtuhumiwa Patrick Tarimo mnamo tarehe 10/08/2020 alijipatia kiasi cha Tsh 20,000,000/= kutoka kwa raia wa kigeni ambapo alimkamata na kujitambulisha kuwa yeye ni afisa usalama wa Taifa na kufanikiwa kujipatia kiasi hicho”alisema Mambosasa

“Kwa upande wa mtuhumiwa Castory Wambura mnamo tarehe 21/08/2020 alitapeli kiasi cha Tsh 15,000,000/= kutoka kwa wafanyabiashara watano wa kariakoo, ambapo alijitambulisha kuwa yeye ofisa wa Polisi na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA)”
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea