Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Manya umeanza leo tarehe 01 Juni, 2018.
Kabla ya uteuzi huo Prof. Manya alikuwa Kamishna wa Madini na alikuwa akikaimu nafasi ya Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini.
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. David Mulabwa kuwa Kamishna wa Madini.
Kwa habari kamili soma hapa chini...






