
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti
Tukio hilo ambalo wengi kupitia mitandao ya kijamii wamedai kuwa ni kimondo na kupelekea maelfu ya wakazi wa Kagera kutoka nje ya nyumba zao kwa kile walichokidhani kuwa ni tetemeko la ardhi kufuatia maafa waliyoyapata septemba 2016.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo, Brigedia Jenerali Gaguti amesema kuwa ameagiza serikali kuwasiliana na baadhi ya wataalamu kwenye mkoa huo ambapo hivi karibuni wanatarajia kutoa tamko kwa umma.
Wakati huohuo mgomo wa madereva wa magari ya abiria uliodumu kwa masaa kadhaa umepatiwa ufumbuzi, baada ya pande mbili zenye mgogoro ikiwemo manispaa pamoja na madereva kukaa meza ya mazungumzo.
Kupitia Katibu tawala wilaya ya Bukoba Kadole Kilugala amesema kuwa katika kikao walichokaa na viongozi wa madereva na wadau wengine wa usafiri, walikubaliana masuala kadhaa ambayo madereva hao wanahitaji yafanyiwe kazi ikiwamo kituo hicho kuwekewa lami