Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla
RC Makalla ametoa agizo hilo wakati wa ziara ya kukagua Miradi huo na kukuta Mkandarasi hayuko eneo la kazi licha ya kulipwa zaidi ya Asilimia 60 ya Fedha huku akimuelekeza Mkandarasi kuongeza Nguvu kazi ili kazi iweze kukamilika na kukabidhiwa kabla ya November mwaka huu.
Aidha RC Makalla amebainisha kuwa Wananchi waliolipwa fidia ya zaidi ya Shilingi Bilioni 6 na bado hawajaondoka, RC Makalla ameelekeza wote waliolipwa kupisha Mkandarasi akamilishe kazi ambapo amesema atapita kila wiki kukagua maendeleo ya Ujenzi.
Mkuu wa Mkoa Dar pia amewataka TARURA kumsimamia Mkandarasi huyo aanze Ujenzi wa Barabara ya mtaa huo ikiwa ni Baada ya kupokea malalamiko ya Wananchi kuhusu ubovu wa Miundombinu ya Barabara hiyo.

